Naibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa leo amesisitiza umuhimu wa amani na usalama barani Afrika, wakati akiwashukuru mabalozi katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kusaidia Umoja wa Mataifa kuangazia suala hilo, na jinsi nchi zote wanachama zinavyoweza kufanya kazi na Muungano wa Afrika AU, kanda zingine na vikundi vya kanda, ili kufanya maisha kuwa salama zaidi katika bara zima.