Nchini Msumbiji katika mji wa pwani wa Palma jimboni Cabo Delgado bado wananchi wanaripoti kusikia milio ya risasi kila uchao, nyumba zao zikitiwa moto na hivyo kulazimika kukimbia maeneo mengine ndani ya nchi yao au hata kuvuka mpaka na kuingia Tanzania, hali inayoendelea kutia hofu kubwa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kuhusu usalama wao.