Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na ongezeko kubwa la vurugu katika eneo linalokaliwa la Wapalestina (oPt) ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa uhasama unaosababisha mashambulio makubwa ya anga ya Israeli huko Gaza, ambayo yalianza tarehe 10 Mei mwaka huu wa 2021 na mapigano katika Ukingo wa Magharibi, pamoja na Mashariki mwa Jerusalem na hiyo kulazimu upelekaji wa misaada ya dharura kama linavyofanya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina, UNRWA.