Ili kuisaidia Lebanon kuondokana na madhara ya janga na kupona vyema, "tutahitaji ushiriki wa kila mtu," Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina Mohammed hii leo ameuambia mkutano wa wafadhili uliofanyika kwa njia ya video ili kuisaidia Lebanon kutokana na mlipuko mkubwa uliotokea katika bandari iliyoko kwenye mji mkuu wan chi hiyo, Beirut na kuwaua watu 150, kujeruhi maelfu na kusababisha uharibifu mkubwa wa sehemu kubwa ya mji.