Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, liko tayari kuanza tena shughuli zake kamili za kibinadamu katika mkoa wa Tigray, Ethiopia mara tu hali itakaporuhusu, kufuatia makubaliano ya kurejesha upatikanaji, ameeleza hii leo msemaji wa shirika hilo Babar Baloch katika mkutano wake na vyombo vya habari mjini Geneva Uswisi.