Wakati shule katika nchi zinazoendelea, zikianza kufunguliwa, shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula, WFP limepokea msaada wa dola milioni 119 kutoka Idara ya kilimo ya serikali ya Marekani ili kusaidia kutoa chakula katika shule kwenye nchi za Asia na Afrika, imeeleza taarifa ya WFP iliyotolewa hii leo mjini Washington Marekani.