Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na wadau wengine wa misaada ya kibinadamu wanaoneza juhudi za misaada kwa ajili ya watu 4,000 ambao ni wakimbizi wa ndani waliopoteza kila kitu katika moto mkubwa uliozuka na kuteketeza kambi ya wakimbizi wa ndani mjini Maiduguri jimbo la Borno Mashariki mwa Nigeria.