Mkutano wa kwanza wa nchi wanachama wa Shirika la Uhamiaji la Umoja wa Mataifa (IOM), kuhusu mbinu jumuishi za uhamiaji na kuoanisha njia za wahamiaji kwenda Ulaya, umefanyika mjini Brussels, Ubelgiji na kuleta matumaini kwa mashirika yanaohusika na wakimbizi na wahamiaji.