Ripoti yenye kurasa 46 iliyotolewa leo mjini Geneva Uswisi na tume ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, UNCHRSS, imeeleza kuwa Sudan Kusini tangu ilipopata uhuru wake mwaka 2013, mzozo wa kikatili nchini humo umesababisha mateso yasiyoweza yasiyopimika kwa raia na kusababisha kiwango viwango vya kutisha vya ukosefu wa chakula na utapiamlo hali ambayo inatumiwa kama mbinu ya vita.