Kamisheni ya Baraza Kuu juu ya Haki za Wanawake, au Kamisheni ya CSW, kabla ya kukamilisha kikao cha mwaka, kwa 2007, ilipitisha mswada wenye mapendekezo manne muhimu: awali, jumuiya ya kimataifa ilitakiwa kuwatekelezea wanawake wa Kifalastina haki halali za kimsingi; pili, watoto wa kike walitakiwa wapatiwe hifadhi bora dhidi ya VVU/UKIMWI; tatu, tabia ya kutahiri mabinti ikomeshwe, na mwishowe, kuhakikisha mila ya kuoza watoto wa kike wenye umri mdogo inasitishwa. Mapendekezo haya manne yanalingana na kiini cha mijadala ya kikao cha 51 cha Kamisheni ya CSW.