Wajumbe watatu kutoka Tume ya Kimataifa ya Wataalamu wa Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa nchini Ethiopia wahitimisha ziara yao ya kwanza nchini Ethiopia, iliyofanyika kuanzia tarehe 25 hadi 30 mwezi Julai walipokwenda kujadili masuala kadhaa kuhusiana na mamlaka yao.
Mtaalam Huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Mali, Alioune Tine, anatarajia kuanza ziara ya wiki mbili nchini Mali kuanzia tarehe 1 hadi 12 mwezi Agosti 2022.
Huku kukiwa na kura 161 za ndio, na nchi nane hazikupiga kura, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha hii leo azimio la kutambua upatikanaji wa mazingira safi, yenye afya na endelevu kama haki ya binadamu kwa wote.
Wachezeshaji maarufu wa muziki duniani kutoka Australia na ambao ni ndugu wameandika wimbo mpya wenye lengo la kuhamasisha kuhusu hatarini wanazokumbana nazo watoto kama vile utumikishaji watoto na usafirishaji haramu wa watoto.
Hebu fikiria machungu yasiyokwisha ya shambulio la kutisha la ukatili wa kingono. Na wakati umefika polisi ukiwa na mikwaruzo mwilini na huku unatetemeka unawaeleza kilichokufika cha kustaajabisha, wao wanakugeuka na kukuuliza: ulikuwa umevaa nini?
Machafuko yanayoendelea nchini Jamhuri ya Afrika ya kati -CAR yanaweza kuwa uhalifu wa kivita imeeleza taarifa iliyotolewa leo na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za binadamu baada ya kuwasilisha ripoti zake mbili za matukio ya kutatanisha yaliyotokea kati ya mwaka 2020 mpaka mwaka huu wa 2022 nchini humo.
Wakati Kenya inajiandaa kufanya uchaguzi mkuu tarehe 9 mwezi ujao wa Agosti, 2022 wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wametoa wito kwa mamlaka nchini humo, wagombea nafasi za uongozi pamoja na vyama vya siasa kuimarisha mazingira wezeshi ili kuepuka ghasia na hatimaye uchaguzi huo ufanyike kwa amani.
Baada ya mamlaka ya Taliban kuwepo madarakani kwa zaidi ya miezi 10 sasa, Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan UNAMA umetoa ripoti yake kuhusu haki za binadamu na masuala mengine nchini humo.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekuwa na mjadala wake wa mwaka kuhusu watoto kwenye maeneo yenye mizozo ambapo Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu watoto hao, Virginia Gamba amewasilisha ripoti ya mwaka ya Katibu Mkuu ambayo iliwekwa bayana kwa umma tarehe 11 mwezi huu wa Julai ikitaja aina sita ya vitendo vibaya zaidi vya ukiukwaji dhidi ya watoto.
Wataalamu huru wa Umoja wa Mataifa hii leo wameyataka mataifa ya Morocco na Hispania kuhakikisha uchunguzi huru unafanyika na hatua kuchukuliwa kwa wale waliohusika na vifo vya waafrika 23 waliokuwa wakijaribu kuvuka mpaka wa Melilla unaotenganisha nchi hizo mbili wakitaka kwenda ulaya.