Nchini Sri Lanka, shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu, UNFPA na shirika moja liitwalo Cheer Up Luv wanafanya kampeni ya pamoja kukabiliana na unyanyasaji wa kingono dhidi ya wanawake kwenye usafiri wa umma.
Katika kipindi cha zaidi ya muongo mmoja waandishi habari takriban elfu moja wameuawa wakati wanafanya kazi yao adhimu, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika ujumbe wake wa siku ya kimataifa ya kukomesha ukwepaji sheria kwa uhalifu dhidi ya waandishi wa habari.