Ukandamizaji dhidi ya waandamanaji unaoendelea nchini Myanmar unaweza kusababisha mzozo kuwa vita kamili sawa na Syria, ameonya leo Kamishina Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, akiyataka Mataifa yenye ushawishi kuchukua hatua za haraka na zenye ufanisi kukomesha mauaji ya raia nchino humo.