Kwenye makala ya awali, ya mfululizo wa vipindi vya sehemu mbili kuhusu Mkataba wa Haki za Mtoto, makala iliotangazwa hapo jana, tulikupatieni mahojiano baina ya mwanafunzi wa kidato cha pili, kutoka Kenya, Millicent Atieno Odondo,
Radhika Coomaraswamy, Mjumbe Maalumu wa KM juu ya Haki za Watoto Walionaswa kwenye Mapigano, ameripotiwa kuwa ana wasiwasi juu ya taarifa alizopokea, zinazoonyesha watoto walio chini ya umri wa utu uzima, wameruhusiwa kujiunga na makundi ya waasi wa katika Sudan.
Josette Sheeran, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Miradi ya Chakula Duniani (WFP), kwenye risala aliotoa mnamo siku ya pili ya Mkutano Mkuu wa Dunia juu ya Udhibiti Bora wa Akiba ya Chakula unaofanyika Roma, Utaliana, alisema raia wote wa kimataifa - na sio viongozi wa dunia pekee - wanawajibika kuhamasishwa wajitayarishe kuwapatia chakula watu bilioni moja ziada wenye kusumbuliwa na tatizo la njaa sugu ulimwenguni.
Navi Pillay, Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu ametoa taarifa yenye kuihimiza Serikali ya JKK kuhakikisha mawakili na watetezi wa haki za binadamu, ikijumlisha waandishi habari, huwa wanapatiwa ulinzi unaofaa utakaowaruhusu kutekeleza majukumu yao, bila ya kuingiliwa kati kikazi wala kubaguliwa, kutishiwa au kulipizwa kisasi kwa sababu ya shughuli zao.
Msemaji wa Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA), Elizabeth Byrs, aliwaambia waandishi habari Geneva, leo hii, kwamba hali ya usalama katika Kivu, Majimbo ya Oriental na Equateur katika JKK, bado inaendelea kuwa mbaya zaidi.
Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) imeripoti ya kuwa vitendo vya uharamia na ujambazi mbaya uliofanyika katika wiki mbili zilizopita, kwenye maeneo ya mashariki katika Chad, ni hali inayohatarisha operesheni za kiutu za kunusuru umma muhitaji.
Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) imeihimiza jumuiya ya kimataifa, kuharakisha michango ya dharura inayotakikana kunusuru maisha kwa raia wa Usomali.
Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) limehadharisha kwamba ulimwengu unakabiliwa na uhaba mkubwa, na wa hatari wa chakula, ulioathiri vibaya sana nchi 31.