Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu, Navi Pillay, kwenye risala yake kuiadhimisha Siku ya Haki za Binadamu, naye pia alitoa mwito wenye kuzihimiza Serikali na watu binafsi, kote ulimwenguni, kuchukua hatua hakika, na za kudumu, kutokomeza na kukomesha janga la ubaguzi milele duniani.