Hivi karibuni Baraza la Umoja wa Mataifa juu ya Haki za Kiutu, lenye wajumbe wanachama kutoka Mataifa 47, lilikutana mjini Geneva, Uswiss kwenye kikao chake cha pili, ambapo kulifanyika majadiliano ya wiki tatu mfululizo kusailia mada kadha wa kadha zinazoambatana na taratibu za kuboresha utekelezaji wa haki za kiutu ulimwenguni.