Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel Dmitry Muratov ambaye alipiga mnada medali yake ya dhahabu ili kuchangisha fedha kwa ajili ya wakimbizi watoto Juni 20, 2022 ameiambia Idhaa ya Umoja wa Mataifa kwamba Kitendo cha medali yake kuvunja rekodi kwa kuuzwa dola milioni 103.5 kimethibitisha kwamba "wakati mwingine ubinadamu unaweza kuja pamoja, na kuoyesha mshikamano".