Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya haki za bindamu, OHCHR, imeelezea wasiwasi wake kufuatia kukamatwa kwa wanaharakati wa kisiasa, wasomi na waliokuwa wabunge, wajumbe wa wilaya na mawakili kwenye jimbo maalum la Hong Kong SAR na kutoa wito waachiliwe huru haraka.