Taarifa ya pamoja kwa vyombo vya habari iliyotolewa hii leo na Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR, pamoja na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la wahamiaji, IOM, la kuhudumia wakimbizi UNHCR na la afya WHO imetoa wito kwa dunia kulinda haki na afya ya wakimbizi, wahamiaji na wasio na utaifa katika wakati huu wa mapambano dhidi ya virusi vya corona, COVID-19.