Kamishna Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet amewasili Bunia, mji mkuu wa jimbo la Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC leo asubuhi kwa saa za huko na kuwa na mazungumzo na Waziri wa Mambo ya haki za binadamu na wajumbe wa kamati ya usalama wa jimbo hilo ambalo hivi hivi karibuni limekuwa limegubikwa na changamoto za kiusalama kutokana na mapigano ya kati ya wahema na walendu.