Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO, Audrey Azoulay amelalamikia mauaji ya wanahabari watatu nchini Mexico, ambao ni Edgar Alberto Nava López, Rogelio Barragán Pérez, na Jorge Ruiz Vázquez, akitoa wito kwa mamlaka kuchunguza matendo hayo yaliyofanywa kati ya mwishoni mwa mwezi Julai na tarehe 2 Agosti.