Taarifa kutoka kwa Geert Cappelaere mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kanda ya Mashariki ya Kati na kaskazini mwa Afrika pamoja na Dkt Ahmed Al Mandhari Mkurugenzi wa Shirika la afya duniani kanda ya Medterania Mashariki iliyotolewa mjini Muscat Oman, Amman Jordan na Cairo Misri inasema nchini Yemen, tangu mwanzoni mwa mwaka huu hadi tarehe 17 mwezi huu wa Machi, takribani watu 109,000 wamekumbwa na ugonjwa wa kuhara na pia vifo 190 vilihisiwa kusababishwa na kipindupindu tangu mwezi Januari.