Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa anayehusika na unyanyasaji wa kingono katika maeneo yaliyokumbwa na vita, amekaribisha na kupongeza hatua ya kutiwa hatia na kwa maafisa kadhaa wa jeshi waliohusika kwenye matukio ya ubakaji katika maeneo ya kaskazini wa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo, akisema kuwa kumbe haki inaweza kupatikana.