Mkataba muhimu wa kufuatilia kupotea kiholela au kwa lazima kwa watu unaanza kutekelezwa leo huku wataalamu wa Umoja wa Mataifa wenye jukumu la kuzisaidia familia kujua hatma ya wapi waliko jamaa zao waliopotea, wameyataka mataifa yote kuhakikisha wanakomesha uhalifu huo kwa kuwafikisha wahusika kwenye vyombo vya sheria.