Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa linakutana hii leo kuzindua rasmi Mpango wa Kimataifa wa Kuchukuliwa Hatua kupambana na biashara haramu ya binadamu. Akizungumza kwenye mkutano huo, Katibu Mkuu Ban Ki-moon anasema biashara haramu ya watu ni miongoni mwa ukiukaji mbaya kabisa wa haki za binadamu.