Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR ambalo linakabiliwa na upungufu mkubwa wa fedha katika shughuli zake nchini Yemen, limeidhinisha mkopo wa ndani wa dola milioni 4.7, ili keundelea na shughuli zake za kuwasaidia maelfu ya wakimbizi wa ndani nchini humo hadi katikati ya mwaka huu.