Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa UM, BI Navi Pillay, ameeleza matumaini yake Ijumatano ya kuwepo na maridhiano miongoni mwa mataifa wanachama kwenye mkutano wa mwezi ujao wa kupambana na ubaguzi, kutokana na kutolewa mswada mpya mfupi wa rasimu ya hati ya mwisho ya mkutano.