Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya kibinadamu na kuratibu misaada ya dharura na waziri wa biashara ya nje na ushirikiano wa maendeleo wa Uholanzi, wamesema hali ya wakimbizi wa ndani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ni mbaya sana na hatua za haraka zahitajika kunusuru watu hao.