Mifumo yote ya ubaguzi wa rangi, chuki dhidi ya wageni na kutovumiliana ni lazima iendelee kupingwa vikali kote duniani. Wito huo umetolewa leo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, katika mjadala maalumu ya maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kutokomeza ubaguzi wa rangi uliofanyika kwenye baraza kuu la umoja wa Mataifa mjini New York Marekani.