Mkutano wa kundi la nchi 20 zinazoongoza kiuchumi duniani, G20 ukianza kesho huko Buenos Aires nchini Argentina, wataalamu wa Umoja wa Mataifa wametaka viongozi hao kupatia suluhu janga la makazi ambalo linawanyima mamilioni ya watu ulimwenguni haki yao ya msingi ya kibinadamu.