Siku ya Jumamosi ya tarehe 7 Aprili mwaka huu wa 2018 ni kumbukizi ya kimataifa kuhusu mauaji ya kimbari nchini Rwanda. Umoja wa Mataifa ulitangaza rasmi mwanzoni mwa mwaka huu siku hii kutambuliwa kimataifa.
Ukeketaji wa watoto wa kike na wanawake unasalia kuwa ni jambo linalotishia tu siyo afya ya kundi hili bali pia maendeleo yao ya kiuchumi, kisiasa na kijamii. Sasa watoto wenyewe wa kike wanasimama kidete kuhakikisha hawakumbwi na kikwazo hicho.