Kitendo cha jeshi kuchukua mamlaka kwa nguvu ni hatua kubwa kurudi nyuma kwa Myanmar, ambayo imekuwa katika njia ya kidemokrasia kwa miaka kumi iliyopita, amesema Naibu Kamishna Mkuu wa Haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Nada An-Nashif wakati wa kikao cha Baraza na haki za binadamu la Umoja wa Mataifa.