Ikiwa bado tunamulika harakati za vyombo vya habari kuendelea kupasha umma habari katika zama hizo za mlipuko wa ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19, nchini Tanzania vyombo vya habari navyo vimechukua hatua kuhakikisha vinaendelea kuhabarisha, kuburudisha na kuelimisha jamii licha ya kuwepo kwa mlipuko huko.