Umoja wa Mataifa umesisitiza kwamba haki za binadamu zinapaswa kuwa muongozo katika hatua zinazochukuliwa kupambana na janga la mlipuko wa virusi vya corona au COVID-19.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa ulimwengu mzima kujifunza kwa nchi ya Rwanda na watu wake kwa namna walivyomudu kuponya majeraha ya athari mbaya za mauaji ya kimbari dhidi ya watutsi.