Hatimaye kikao cha kwanza cha mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kimeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani chini ya uongozi wa Rais wake Balozi Tijjani Muhammad-Bande kutoka Nigeria.
Baraza la haki za binadamu leo limefungua pazia mjini Geneva Uswis huku kamisha mkuu wa Haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa akionya kwamba moto wa nyika unaoendelea kusambaa Amazoni “kimsingi tunautekeleza mustakabali wetu”.