Kuelekea siku ya kimataifa ya kumbukizi ya manusura wa ugaidi, ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabiliana na ugaidi UNOCT imechukua hatua ya kupaza sauti za manusura hao kutoka maeneo mbalimbali duniani akiwemo mwanamke mmoja raia wa Cameroon ambaye anasema alilazimika kuwavisha mavazi ya kike watoto wake wa kiume ili wasichukuliwe na magaidi wa Boko Haram.