Tuzo ya kila mwaka ya shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi, UNFPA ambayo hutolewa kwa mtu binafsi na shirika au taasisi inayojikita katika kuboresha afya ya uzazi kwa wanawake, pamoja na afya ya akina mama na wajawazito, mwaka huu imeenda kwa Emma Theofelus ambaye ni Naibu Waziri wa Habari wa sasa nchini Namibia na mshindi wa kwanza mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kupata tuzo hiyo.