Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake wa kuadhimisha maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Tafakari kuhusu Mauaji ya Kimbari ya mwaka 1994 Dhidi ya Watutsi nchini Rwanda.alioutoa kwa njia ya video, amesema wakati huu dunia inapojiunga katika mshikamano na watu wa Rwanda, ni lazima kuangalia sana ulimwengu wa leo na kuhakikisha kwamba tunazingatia masomo ambayo wanadamu waliyapata kutokana na tukio hilo la miaka 27 iliyopita ambapo zaidi ya watu milioni moja waliuawa.