Msemaji wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric amesema ofisi ya mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC-(MONUSCO) imepokea madai mengine ya miendendo mibaya ikiwemo unyanyasaji wa kingono, ukiwahusisha walinda amani kutoka Afrika Kusini.