Mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, la Uhamiaji, IOM, la kuhudumia watoto, UNICEF na Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, OHCHR, wamesikitishwa sana na taarifa za kifo cha mtoto mchanga kilichotokea Jumapili wakati wa walinzi wa mpaka wa pwani wa Trinidad walipokuwa wanakizuia chombo kilichowabeba wavenezuela waliojaribu kuvuka mpaka wa kusini mashariki mwa visiwa hivyo vilivyoko katika bahari ya Karibea.