Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet leo ameelezea kusikitishwa kwake na idadi kubwa ya Wapalestina, wakiwemo watoto, waliouawa na kujeruhiwa katika ardhi ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu mwaka huu, ikiwa ni pamoja na uhasama mkali unaoendelea kati ya Israel na makundi ya wapalestina wenye silaha huko Gaza mwishoni mwa juma lililopita.