Katika siku ya tatu ya ziara yake rasmi nchini China, kamishina mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet amelezea kuwa ni fursa muhimu ya kuangazia masuala ya haki za binadamu na shuku na shaka katika mazungumzo yake na Rais Xi Jinping na maafisa wengine wakuu wa serikali , ikiwa ni ziara ya kwanza ya aina hiyo kufanywa na mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa tangu mwaka 2005.
Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Michelle Bachelet ametoa taarifa leo akisema amesikitishwa na uamuzi ulioripotiwa wa Taliban kuvunja tume huru ya Haki za Kibinadamu ya nchi hiyo.
Miaka sita iliyopita, yaani mwaka 2016, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa aliunda Mfuko wa kufadhili miradi inayolenga kusaidia waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia na hata watoto waliozaliwa kutokana na ukatili wa kingono uliofanywa na baadhi ya wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wakiwemo walinzi wa amani au watu wengine wanaohusika na shughuli za Umoja wa Mataifa katika mataifa mbalimbali.
Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu, MichelleBachelet, amesema anatiwa hofu na kusikitishwa sana na madhara makubwa ya haki za binadamu kutokana na kuongezeka kwa machafuko na ghasia zinazohusisha magenge yenye silaha nzito nzito huko Port-au Prince, nchini Haiti.
Upatikanaji wa vifaa vya usaidizi kwa nchi masikini ni asilimia 3
Upatikanaji wa vifaa vya usaidizi kwa nchi tajiri ni asilimia 90
Iwapo vinapatikana hususan kwa watoto wenye ulemavu vinasaidia kubadili maisha yao na familia zao
Ripoti mpya iliyotolewa leo na mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa lile la afya ulimwenguni WHO na la kuhudumia watoto UNICEF imefichua kuwa zaidi ya watu bilioni 2.5 wanahitaji kifaa kimoja au zaidi cha usaidizi, kama vile viti mwendo, vvifaa vya usaidizi wa kusikia au programu zinazosaidia mawasiliano na utambuzi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres Jumapili ametoa wito wa kujitolea zaidi ili kuhakikisha maelewano na utangamano katika jamii siku moja baada ya watu 10 kuuawa, na watatu kujeruhiwa, katika shambulio la ubaguzi wa rangi kwenye duka kubwa huko Buffalo, New York.
Uchunguzi lazima ufanyike dhidi ya hatua zinazochukuliwa na vikosi vya usalama vya Israel, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Michelle Bachelet amesema Jumamosi, akitoa wito wa uwajibikaji na kukomeshwa kwa tabia ya watu kutoadhibiwa.
Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO Qu Dongyu ametoa wito kwa nchi tajiri zaidi duniani G7 kusaidia kukabiliana na uhaba wa chakula katika siku zijazo kwani vita inayoendelea nchini Ukraine imepunguza usambazaji na kupandisha bei juu katika viwango vya kuvunja rekodi na kuyaweka mashakani mataifa ambayo tayari yana hatari ya kuathirika kote barani Afrika na Asia.
Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu Michelle Bachelet amesema ofisi yake imethibitisha matukio ya ukatili wa kingono dhidi ya wanawake nchini Ukraine, ambako mapigano yanaendelea tangu uvamizi uliofanywa na Urusi kuanzia tarehe 24 mwezi Februari mwaka huu.