Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, OHCHR, imeelezea wasiwasi wake kuhusu kuendelea kwa ukosefu wa usalama, umaskini, ukosefu wa usawa na kuongezeka kwa uhasama wa kisiasa ambao huenda ukachochea ghadhabu kutoka kwa umma ambayo itafuatiwa na kukandamizwa na polisi na ukiukaji wa haki za binadamu.