Katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya kuadhimisha waathirika wa matendo ya vurugu yanayotokana na dini au imani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ulimwengu unapaswa kupinga na kukataa wale ambao kwa mabavu na kwa uongo wanashawishi kujenga imani potofu, kuchochea mgawanyiko na kueneza hofu na chuki.
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J.Mohammed ameshiriki mkutano wa mtandao wa wanawake viongozi barani Afrika, AWLN, akipongeza mtandao huo kwa kuchuuka hatua za kuleta pamoja viongozi wanawake wastaafu, wale wa sasa na viongozi vijana.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesema miaka miwili ya harakati za kila uchao za kujikwamua kimaisha kwa warohingya waliosaka hifadhi nchini Bangladesh zimetumbukiza nyongo mustakabali wa elimu kwa kizazi kizima
Mradi wa Quid unaoendeshwa na wanawake mjini Verona Italia katika sekta ya fasheni mbali ya kushughulikia changamoto za mabadiliko ya tabia nchi pia umekuwa neema kubwa kwa kuwapa ajira wanawake wenye Maisha duni.
Umoja wa Mataifa umesema changamoto mbalimbali ikiwemo migogoro ya mara kwa mara inayoshuhudiwa katika baadhi ya nchi ubora wa elimu, umasikini na hata mazingira vinakwamisha vijana wengi kupata elimu
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya watu wa asili inayoazimishwa kila tarehe 9 Agosti ya kila mwaka, ambapo maadhimisho yanaenda sambamba na mwaka 2019 ambao ni mwaka wa kimataifa wa lugha za asili ikilenga kusaka hatua za haraka kulinda, kuchagiza na kuendeleza lugha za asili.
Lugha za asili zikiwa hatarini kutoweka, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaka hatua zaidi kulinda lugha hizo na haki nyinginezo za kundi hilo.
Kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani hii leo Naibu Katibu Mkuu wa chombo hicho Amina J. Mohammed ameongoza tukio la maadhimisho ya siku ya watu wa asili, ambayo maudhui yalikuwa lugha za asili.
Lugha za asili zikiwa hatarini kutoweka, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaka hatua zaidi kulinda lugha hizo na haki nyinginezo za kundi hilo. Jason Nyakundi na taarifa zaidi.