Hii leo kwenye mji wa Bonn, Ujerumani wajumbe wa kimataifa wamekusanyika tena kwenye duru nyengine ya kikao kisio rasmi, kushauriana juu ya maafikiano yanayotakikana kukamilishwa kwenye Mkutano Mkuu ujao, wa kupunguza umwagaji wa hewa chafu ulimwenguni, utakaofanyika mwezi Disemba mjini Copenhagen, Dennmark.