Njaa imeongezeka katika eneo la kusini la Madagascar, mfululizo wa miaka ya ukame inazidisha mateso ya maelfu ya watu, kuharibu mavuno na kuzuia watu kupata chakula, limeeleza shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa, WFP.
Wiki hii shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM limetoa ombi la dola milioni 2 ili kuhakikisha linaendelea kuwa na fursa ya kufikisha misaada ya kibinadamu ya kuokoa maisha kwa watu waliohatarini zaidi na jamii zinazowahifadhi.
Wataalam wa WMO wameeleza kuwa licha ya kupungua kwa uzalishaji wa viwandani kwa sababu ya janga la COVID-19 na karantini, mkusanyiko wa hewa ya ukaa, CO2 angani bado uko juu.