Watu 650,000 wameathirika na mafuriko yanayoendelea nchini Sudan kufuatia mvua kubwa zilizoanza kunyesha tangu mwezi Julai na juma hili pekee watu wengine 110,000 wametawanywa na sasa wanahitaji msaada wa haraka wa kibinadamu limesema shirika la Umoja wa Mataifa la msaada wa kibinadamu na masuala ya dharura OCHA.