Mkurugenzi Mkuu wa shirika la nishati ya atomiki duniani, IAEA, Yukia Amano, aaga dunia, siku chache tu kabla ya kuwasilisha barua yake ya kujiuzulu wadhifa huo. Suala la wahamiaji na wakimbizi wanaosaka maisha bora barani Ulaya kupitia Mediteranea lapigiwa chepuo kwa hatua mpya chanya barani humo. Nchini Kenya mradi mpya kwenye pwani ya nchi hiyo washamirisha mikoko na biashara ya hewa ya ukaa. Baa la nzige latishia mustakabali wa chakula kwenye pembe ya Afrika na Yemen, na mtoto Mwigulu ambaye alikatwa mkono kisa tu ni albino azungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa.