Kulingana na tamwimu za Umoja wa Mataifa ni kuwa karibu watu 300,000 waliuawa na majanga ya kiasili mwaka 2010 wakati baadhi ya majanga mabaya zaidi yakiwa ni pamoja na tetemeko la ardhi lililotokea nchini Haiti na kusababisha vifo vya watu zaidi ya watu 222,000 na joto nchini Urusi pamoja na moto wa msituni vilivyosababisha vifo vya watu 56,000.