Wiki iliopita KM Ban Ki-moon, alizuru ukingo wa ncha ya Kaskazini ya dunia, kwenye eneo la Akitiki, ambapo alishuhudia mwenyewe athari kubwa za mabadiliko ya hali ya hewa na kujionea, binafsi, namna miamba ya barafu na michirizi ya barafu inavyoyayuka kwa kasi kabisa kwenye eneo hilo, hali ambayo inachochea kina cha bahari kunyanyuka katika sehemu kadha za dunia, na kuhatarisha baadhi ya mataifa ya visiwa ambavyo huenda vikaangamia ikiwa hali hii haotidhibitiwa mapema.