Shirika la UM juu ya Ilimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) jana lilimaliza Mkutano wa Dunia juu ya Iimu ya Juu uliofanyika Paris, ambapo kulitolewa mwito maalumu unaozitaka nchi wanachama kuongeza mchango wao katika juhudi za kukuza ilimu. Kwenye taarifa rasmi ya mkutano, wajumbe waliowakilisha nchi 150 walitilia mkazo umuhimu wa kuwekeza posho ya bajeti lao kwenye sekta ya ilimu, ili kujenga jamii yenye maarifa anuwai, na inayomhusisha kila raia, ambaye atapatiwa fursa sawa ya kushiriki kwenye tafiti za hali ya juu, huduma itakayowakilisha uvumbuzi na ubunifu wenye natija kwa umma.